NAFASI YA VIJANA KUJIKWAMUA KIUCHUMI UKIW
BADO MASOMONI
Ni
matumaini yangu kuwa ndugu msomaji wa Makala hii mzima na buheri wa afya, kama
ilivyo ada tunaangazia masuala mbalimbali
yanayotuhusu sisi vijana ni katika namna ya kuhakikisha tunakua na
mtazamo chanya katika jamii inayotuzunguka. Leo tutaangazia suala la kujikwamua
kiuchumi hasa wakati vijana wanapokua masomoni.
Linaweza
kuwa si jambo geni kwako kusikia wanafunzi wa vyuo mbalimbali hapa nchini wanamiliki
vitega uchumi, hiyo ni kuhakikisha tu wanafanya jitihada za kila namna kutoka
kimaisha hususani ukizingatia suala la ajira nchini bado ni kitendawili kisicho
na majibu.lakini pia katika kuhakikisha hawakosi fedha ya malazi wanapokua
vyuoni.
Tanzania
kama ilivyo nchi nyingi za kiafrika zinazoendelea inakabiliwa na tatizo kubwa
la ajira hasa ukizingatia tatizo la ajira kwa vijana linakadiriwa kuwa Zaidi ya
vijana elfu 70,000 wanaohitimu kutoka vyuo vikuu ni asilimia kumi tu (10%)
wanaopata nafasi ya ajira, kitu kinachosababisha vijana wengi wanaomaliza
masomo yao ya elimu ya juu kubaki mitaani wakilalamika bila kazi.
Kuna kilio
ambacho kila unapogusia suala la ujasiliamari basi vijana wengi wa vyuo vikuu
utasikia wakilia na kulalamikia suala la mitaji, Vijana wengi wana mawazo ya
kufanya biashara, lakini wakifikia kwenye suala la mitaji wengi hukwama, wengi
huamini kuwa wanahitaji mitaji ya million kadhaa ili kufanya biashara kitu
ambacho kinarudisha harakati zao za kujikwamua kiuchumi nyuma
Fikra hizo za vijana naweza sema si sahihi
sana kwani unaweza kuanza hata na mtaji wa elfu ishirini mpaka laki moja na
ukatoka pia, lakini pia unaweza tumia kipaji ulichonacho kutoka kimaisha, hapa
ndipo ule usemi wa” tone na tone hujaza ndoo” unapochukua nafasi yake. Kitu cha
msingi cha kuzingatia hasa wewe kama kijana ni kuwa na mipango madhubuti na
endelevu katika shughuli zako
Unaweza shangaa
na kujiuliza mtu anawezaje kutoka kwa mtaji wa shilingi elfu ishirini? Hyo hiyo
pesa ya matumizi unayopata kutoka nyumbani inaweza kukuinua kutoka ngazi moja
hadi nyingine ya kimaendeleo Lakini haya yote yanawezekana ukiwa na mipango
madhubuti, na yote haya tutapata kuyaangazia katika matoleo yanayofuata,
usikose
Kwa maoni na ushauri: 0656 249607, au elvinecb@gmail.com. Asanteni.
0 comments:
Post a Comment